Pages

Monday, 12 November 2012

Simba kimenuka tena



WAKATI mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara, Simba jana wakipokea kichapo cha pili mfululizo, Kocha Mkuu, Milovan Cirkovic amevunja ukimya na kuulalamika uongozi kutomshirikisha katika maamuzi yaliyomng’oa kikosini beki Juma Nyoso.
Akizungumza baada ya pambano hilo, Milovan aliutupia lawama uongozi wa Simba kwa kumshusha Nyoso bila kumshirikisha na kuchangia kuidhoofisha safu ya ulinzi na timu kwa ujumla, huku akikiri wazi kudhihiri kwa pengo la mlinda mlango wake, Juma Kaseja.
Kauli ya Milovan na misimamo wa mashabiki, umezua hali ya sintofahamu klabuni, ambapo mabango ya kumtaka Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kuachia ngazi yalionekana, ambapo mashabiki wa tawi la Simba Vuvuzela, walionesha bango lililoandikwa ‘Simba bila Kaburu inawezekana.’
Ndani ya uwanja, Simba kama ilivyokuwa kwa washindi wa pili wa msimu uliopita Azam FC, kwa pamoja zimeshindwa kuing’oa Yanga katika kilele cha ligi hiyo, baada ya zote kujikuta zikipokea vichapo kwenye viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam na Mkwakwani jijini Tanga.
Katika mechi hizo za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14, Simba imeendeleza matokeo mabovu, safari hii ikiwa Uwanja wa Taifa, baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Toto Africans, huku Azam ikichapwa mabao 2-1 na Mgambo JKT ya Handeni.
Simba iliingia uwanjani ikiwa nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kwa pointi zao 23, moja nyuma ya Azam iliyoingia dimbani ikiwa nafasi ya pili kwa pointi 24 – zote zikipania ushindi ili kuing’oa Yanga iliyokaa kileleni ikiwa na pointi 26.
Jijini Dar es Salaam, pambano lilianza kwa kasi na mashambulizi ya hapa na pale, ambapo Nassor Masoud ‘Cholo’ alionywa kwa kadi ya njano mapema dakika ya nane, kutokana na rafu yake kwa mchezaji wa Toto wakati wakiwania mpira.
Dakika ya 11, Amri Kiemba alishindwa kuipa Simba bao baada ya shuti yake kudakwa na kipa Erick Ngwengwe, wakati dakika ya 24, Felix Sunzu nae alikosa bao baada ya mpira wake wa kichwa kugonga mwamba na kudakwa na kipa huyo.
Simba ilizidi kushambulia lango la Toto na kiungo Mussa Said alifanya kazi ya ziada katika dakika ya 40, alipookoa mpira uliopigwa na Kiemba, huku mlinda mlango Ngwengwe akiwa amepotea maboya.
Hadi filimbi ya mapumziko ya mwamuzi Judith Gamba wa Arusha, si Simba wala Toto waliofanikiwa kutikisa nyavu, licha ya Wekundu wa Msimbazi kushambulia mara kadhaa.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na mashambulizi ya kila upande, ambapo Mussa Said, aliipatia Toto bao katika dakika ya 73 kwa kichwa, akiunganisha mpira wa adhabu ndogo wa Mohammed Jingo.
Bao hilo lilipokelewa kwa shangwe na mashabiki wa Yanga, ambao licha ya upinzani wa jadi uliopo dhidi ya Simba, lakini pia ina undugu na Toto.
Kwa ushindi huo Toto imeongeza pointi zake kutoka tisa hadi 12, ingawa imesalia kwenye nafasi ya 12 baada ya Mgambo nao kuwachapa Azam.
Simba: William Mweta, Nassor Masoud ‘Cholo,’, Paul Ngalema, Komanbil Keita, Shomari Kapombe, Jonas Mkude, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi na Mrisho Ngasa.
Toto: Erick Ngwengwe, Ally Ahmad, Erick Marilo, Everist Maganga, Peter Mutabuzi, Msafiri Hamisi, Mussa Saidi, Emmaanuel Swita, Kheri Mohammed, Selema Kibuta na Mohammed Jingo.
Kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, mabao mawili kutoka kwa Issa Kandulu na Nassor Gumbo, yalitosha kuipa pointi tatu muhimu Mgambo JKT, huku Kipre Tchetche akiifungia Azam bao la kufutia machozi na kudumisha mwendo wa kusuasua.
Licha ya jitihada za Azam kutaka kubadili hali ya mambo katika timu yao, Mgambo ikafanikiwa kuwazima kwa bao la Gumbo la dakika ya 78, akiyemalizia pasi ya kifua ya mfungaji wa bao la kwanza, Kandulu.
chanzo:daima

Milovan asema kaseja kipa bora Tanzania.

KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic, amemtangaza kipa wake Juma Kaseja kuwa ni kipa bora zaidi kwenye kikosi chake kinachoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara na Tanzania kwa ujumla.
Milovan alitoa kauli hiyo juzi mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu ya Bara kati ya timu yake dhidi ya Toto African mchezo ambao Simba ililala kwa bao 1-0.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Milovan raia wa Serbia alisema kwa upande wake, Kaseja ndiye kipa bora zaidi Simba na hapa nchini.
Milovan alisema, ubora na umuhimu wake umeonekana kwenye mechi na Toto baada ya kipa namba mbili wa timu hiyo, Wilbert Mweta, kudaka na kufungwa bao la kizembe.
“Mmeona kilichotokea, kipa kafanya uzembe timu imefungwa, siwezi kusema ni yeye mwenyewe kaifungisha timu kwa kuwa timu inapoteza ikiwa na wachezaji 11 uwanjani, lakini kwangu Kaseja ni kipa bora.
“Namhitaji kwenye kikosi changu, ni bora siyo Simba tu bali nchi nzima.
“Umuhimu wake umethibitika leo hii katika mechi na Toto, tumefungwa bao kutokana na uzembe, angekuwa Kaseja sidhani kama tungefungwa,” alisema Milovan.
Kaseja, katika mechi ya ligi dhidi ya Mtibwa Sugar iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, alishutumiwa kuihujumu timu baada ya kufungwa mabao mawili katika mchezo huo uliomalizika kwa Simba kufungwa mabao 2-0.
chanzo:.globalpublisher

76 not out: Messi closing in on Muller after breaking Pele's record for most goals in a calendar year



Lionel Messi has passed Pele’s milestone of goals in a calendar year by scoring for the 75th and 76th time in 2012.
The Argentine moved within nine of Gerd Muller’s all-time record and helped Barcelona win 4-2 at Mallorca in La Liga. 
Xavi Hernandez scored in the 28th minute before Messi struck in the 44th. Cristian Tello added a third goal a minute later.
Mallorca replied twice but Messi made it 4-2 as Barcelona rebounded from their surprising 2-1 defeat at Celtic in the Champions League. 
Pele scored 75 goals in 1958. Muller netted 85 in 1972.
Muller will perhaps be discouraged to hear that Messi is chasing another of his records having already surpassed one last season.
The prolific German hitman scored 67 goals for Bayern Munich in the 1972-73 season. 
This remained the highest tally in a European club season until the diminutive Messi scored 73 for Barcelona in the 2011-12 campaign.
Messi has nine games left to score the ten goals to surpass Muller's 85 goals, and given his current run of form - 15 goals in 11 La Liga games - the 25-year-old is on course to usurp the German once more.
The striker set another record last season when he scored 50 goals in a La Liga season, moving to the top of Barcelona's all-time top goalscorer list in the process after surpassing Cesar Rodriguez’s 57-year milestone of 232 goals in March. 
Barcelona manager Tito Vilanova expressed his delight at Messi's strike rate.
He said: 'Leo’s records are spectacular. It’s spectacular when you think that he scores so many goals. 
'Some few players reach these numbers in seven or eight seasons, he does it in one. And most of his goals are great goals.'
La Liga champions Real Madrid were indebted to goals from Cristiano Ronaldo and substitute Alvaro Morata in a 2-1 win at waterlogged Levante.
Ronaldo sustained a nasty cut above his left eye when he was caught by David Navarro’s elbow in Valencia but still went on to score.


 http://www.dailymail.co.uk/