Pages

.

Monday 24 March 2014

Chelsea vs Arsenal 6-0 ~ All Goals & Highlights (22/03/2014

Wednesday 22 May 2013

Siku Yanga alipomaliza ligi kwa ushindi dhidi ya mpinzani wake wa jadi S...

Wednesday 8 May 2013

Britain's most successful football manager calls it a day: Sir Alex Ferguson RETIRES after 27 years at Manchester United


Manchester United manager Sir Alex Ferguson today announced that he will retire from the club at the end of the season after 27 years in charge.
The 71-year-old clinched his 13th Premier League title with the club last month, but that will be his last hurrah as manager of the Old Trafford club.
Speculation had been rife that the fiery Scotsman would end his long tenure at the club, but Manchester United chiefs had refused to comment.
Sir Alex said in a statement that it was important to him to leave the club in the 'strongest possible shape.'
He said: 'The decision to retire is one that I have thought a great deal about and one that I have not taken lightly. It is the right time.
'It was important to me to leave an organisation in the strongest possible shape and I believe I have done so.

Monday 11 March 2013

Full Torres falls and Ferdinand being a poor sport - Manchester United v...


Watch Barnes's trip on referee Miller from 50 seconds in


Ubingwa wanukia Yanga



MABINGWA mara 23 wa Tanzania bara tangu mwaka 1965, Yanga, jana walizidi kujisafishia njia kuelekea ubingwa msimu huu baada ya kuwanyuka Toto African bao 1-0.
Kwa ushindi huo, Yanga chini ya Kocha Ernie Brandts wamefikisha pointi 45, hivyo kuzidi kukalia uongozi wa ligi ikifuatiwa kwa karibu na Azam yenye pointi 37.
Yanga walianza kulikaribia lango la ndugu zao Toto dakika ya 37, lakini Jerry Tegete, mtoto wa Meneja wa Uwanja wa CCM Kirumba, akashindwa kuitumia vizuri nafasi hiyo.
Kabla ya hapo, dakika ya 33 Erick Mlilo wa Toto alilimwa kadi ya njano na mwamuzi Endrew Shamba wa Pwani kwa mchezo mbaya.
Dakika ya 44, Emmanuel Swita pia wa Toto alilimwa kadi ya njano kwa mchezo mbaya.
Hadi mapumziko hakuna timu iliyokuwa imepata bao licha ya kuwepo kwa mashambulizi makali kwa timu zote.
Yanga walikianza kipindi cha pili kwa mashambulizi makali, lakini mabeki wa Toto walikuwa makini kuokoa hatari.
Dakika ya 47 na 53, Simon Msuva alipata nafasi ya kufunga kutokana na kazi nzuri ya Hamis Kiiza, lakini alishindwa kufanya hivyo.
Toto walimtoa Mohamed Jinga na kuingia Hery Mohamed dakika ya 63, pia wakamtoa Selemani Kibuta na kuingia Chika Oulge.
Dakika ya 68, Mlilo alilimwa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Msuva.
Yanga walimtoa Tegete dakika ya 74 na kuingia Nizar Khalfan ambaye dakika nne baadae aliifungia timu yake bao hilo pekee kwa kichwa akiunganisha krosi maridadi ya Kiiza.
Dakika ya 83, Kiiza alikosa bao baada ya shuti yake kupaa juu ya lango kabla ya Msuva naye kushindwa kufunga dakika ya 86.
Yanga wanapaswa kujilaumu wenyewe kwa kushindwa kuzitumia nafasi walizopata.
Wakati Yanga ikizidi kupasua anga kuelekea ubingwa, washindani wao wa karibu, Azam jana walivutwa shati na Polisi Moro kwa kutoka sare ya bao 1-1 Uwanja wa Chamazi.
Matokeo hayo yameipa Yanga nafasi ya kuongoza kwa tofauti kubwa ya pointi nane, kwani wakati Azam ikifikisha pointi 37, Yanga inatanua kileleni kwa pointi 45.
Yanga: Ally Musa, Godfrey Taita, David Luhende, Mbuyu Twite, Kelvin Yondan, Athuman Idd ‘Chuji,’ Simon Msuva, Frank Domayo, Jerry Tegete/Nizar Khalfan, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima.
Toto: Erick Ngwege, Erick Mlilo, Robert Magadula, Erick Kyaruzi, Everist Maganga, Hamis Msafiri, Severine Constatine, Emmanuel Swita, Chika Olugbe, Musa Musa/Simba Boaz na Mohamed Jinga/Hery Mohamed.
chanzo:daima

Sunday 3 March 2013

Simba mwaka wa taabu, Azam FC yafanya kweli


TIMU ya Simba, jana, iliaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao na Libolo ya Angola katika mechi ya marudiano ya hatua ya awali ya michuano hiyo yenye utajiri mkubwa kwa ngazi ya klabu.
Kwa kipigo hicho, Simba chini ya kocha wake Mholanzi, Patrick Liewig, wameaga kwa kulimwa jumla ya mabao 5-0.
Katika mechi ya kwanza iliyopigwa wiki mbili zilizopita Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, walifungwa bao 1-0.
Hata hivyo, dalili za kung’olewa mapema kwa Simba iliyowahi kufika hatua ya nane bora ya michuano hiyo mwaka 2003, zilionekana mapema kwa kuonyesha kiwango butu chini ya Liewig aliyeitwaa timu hiyo Novemba mwaka jana kutoka kwa Mserbia, Milovan Cirkovic.
Wakati Simba ikiangukia pua, wawakilishi wengine kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Azam FC, wameitoa Tanzania kimasomaso kwa kutinga raundi ya kwanza baada ya kuwang’oa Al Nasr Juba ya Sudan Kusini. Baada ya kushinda mabao 3-1 katika mechi ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, Azam jana walidhihirisha ubora wao kwa kuwafunga wapinzani wao 5-0, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 8-1.
Wafungaji kwa upande wa Azam katika mechi ya jana iliyochezwa mjini Juba, ni John Bocco aliyefunga mabao mawili na Hamis Mcha naye aliyefunga mawili huku moja likifungwa na Kipre Tchetche, nyota wa kimataifa wa Ivory Coast.
Matokeo hayo ni faraja kubwa kwa wachezaji, viongozi, wapenzi na mashabiki wa timu hiyo ambayo ni mara ya kwanza kwao kushiriki michuano ya kimataifa tangu kuanzishwa kwao Juni 24, mwaka 2007.
Azam waliipata nafasi hiyo baada ya kumaliza nafasi ya pili katika msimu uliopita nyuma ya Simba iliyokuwa bingwa huku Yanga ikiwa ya tatu, hivyo kukosa tiketi ya kucheza michuano ya kimataifa.
chanzo:Daima